Majukumu

  1. Kuwapatia Watanzania fursa za kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi;
  2. Kuandaa Mpango Mkakati wa sekta na kisekta na kuhamasisha matumizi ya rasilimali kwa shughuli za Uwezeshaji wa Wananchi;
  3. Kuhamasisha na kuhimiza uwekaji wa akiba, uwekezaji, na ushirikishwaji makini wa Wananchi kwenye shughuli za Kiuchumi;
  4. Kuandaa Mkakati wa kitaifa Uraghibishi wa sekta mbalimbali wa shughuli za uwezeshaji wananchi kiuchumi;
  5. Kuendeleza na kuwezesha shughuli za kibiashara zilizoanzishwa na kuendeshwa na watanzania;
  6. Kuainisha fursa za mafunzo ya kiuchumi na uwekezaji na kuratbu programu za mafunzo hayo;
  7. Kusimamia, kuongoza na kutafuta vyanzo vya fedha kwa ajili ya Mfuko wa Uwezeshaji;
  8. Kuhamasisha utafiti wa shughuli za kiuchumi na kuhimiza ushirikiano na Taasisi za utafiti;
  9. Kufanya mapitio ya sheria mbalimbali kwa lengo la kutoa mapendekezo ambayo yatalenga kuboresha mazingira ya uwezeshaji wananchi kiuchumi;
  10. Kuandaa mfumo wa kufuatilia maendeleo ya shughuli za kiuchumi na kutathimini matokeo; na mfumo wa menejimenti ya habari za uwezeshaji;
  11. Kushauri kwenye shughuli zote za uanzishaji wa vikundi, ushirika, ushirikiano na ushirikiano wa biashara wa muda mfupi;
  12. Kuanzisha mfumo wa utoaji taarifa za uwezeshaji wa wananchi kiuchumi kutoka sekta zote.