Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
Baraza linatoa huduma za mafunzo, ushauri wa biashara, na kusaidia wajasiriamali kuboresha matumizi ya mikopo yao kwa kuhakikisha wanapata maarifa ya usimamizi wa fedha na uendeshaji wa biashara. Pia, linawasaidia wajasiriamali kufikia masoko mapya na kufanya biashara zao kuwa endelevu.
Baraza linafanya kazi ya kuwaunganisha (link) wajasiriamali, wakulima, wafugaji, na makundi mengine ya kiuchumi na mifuko na programu za uwezeshaji ili waweze kupata mikopo kwa urahisi na msaada wa kifedha kwa ajili ya shughuli zao za uzalishaji.
Baraza linafanya ufuatiliaji wa mara kwa mara na kufanya vikao na wajasiriamali pia linashirikiana na taasisi za kifedha na mifuko ya uwezeshaji kuhakikisha kuwa wajasiriamali wanapata mikopo kwa urahisi kwa kutoa urahisi wa mchakato wa maombi, kuondoa vikwazo vya kifedha kama vile dhamana, na kutoa...
Wajasiriamali wanapata faida mbalimbali ikiwa ni pamoja na mikopo ya riba nafuu, mafunzo ya biashara, ufanisi katika uzalishaji, na upatikanaji wa masoko kwa bidhaa zao. Hii inawasaidia kukua na kuimarisha biashara zao, na pia kuwa na uwezo wa kuajiri watu na kuchangia katika uchumi wa taifa.
Baraza linajitahidi kufikisha huduma za mifuko na programu za uwezeshaji kwa wajasiriamali wa maeneo ya vijijini kwa kushirikiana na Halmashauri za wilaya na mashirika yasiyo ya kiserikali. Hii inajumuisha mafunzo, huduma za kifedha, na mifumo ya usambazaji wa mikopo kwa maeneo ya mbali. Pia, Baraza...
Baraza kwa kushirikiana na wadau linatoa mafunzo ya ujasiriamali, ushauri wa kifedha, na msaada wa kiufundi kwa wajasiriamali wanaoanzisha au kuendeleza biashara zao. Pia linashirikiana na taasisi nyingine kutoa elimu kuhusu namna ya kuandika mipango ya biashara na jinsi ya kufikia mifuko ya uwezesh...
Baraza linashirikiana na mifuko na programu za uwezeshaji zinazolenga kuwasaidia kiuchumi wajasiriamali. Kwa mawasiliano zaidi kujua aina za mifuko na programu za uwezeshaji, tembelea tovuti ya Baraza: https://www.uwezeshaji.go.tz  
Kwa kushirikiana na wadau mbalimbali Baraza linahamasisha na kutoa elimu kwa wajasiriamali kuhusu mifuko na programu za uwezeshaji zilizopo. Pia, linatoa taarifa sahihi kuhusu vigezo na masharti ya mikopo ili wajasiriamali waweze kufikiwa na mifuko hii kwa urahisi na kuelewa jinsi ya kuitumia kwa uf...
Baraza linatoa msaada kwa wajasiriamali kwa kuwaunganisha na taasisi za kifedha ambazo zinatoa mikopo kwa masharti nafuu, huku pia likitoa elimu kuhusu njia mbalimbali za kuhakikisha dhamana kwa mikopo, kama vile kutumia mali zao au kushirikiana na wadhamini wa nje.
Ndiyo, wajasiriamali wanaweza kushirikiana kwa kuunda vikundi vya kijasiriamali na kuwasilisha maombi ya mkopo kwa pamoja. Hii inasaidia kuwa na ushirikiano wa kisera, kuongeza fursa ya kupata mikopo, na kufanikisha maendeleo ya biashara kwa pamoja
Feedbacks

Mrejesho, Malalamiko au Wazo