Imewekwa: 01 Jul, 2026
Baraza la Taifa la Uwezeshaji Kiuchumi (NEEC) limeendelea kutoa huduma katika maonesho ya 50 ya biashara ya Kimataifa yajulikanayo kama Sabasaba.
Wananchi wameendelea kupata huduma katika banda la Baraza linalopatikana katika banda kuu la Ofisi ya Waziri Mkuu.
Afisa Uwezeshaji kutoka Baraza Bi. Minaeli Kilimba amewaomba Watanzania kujitokeza kwa wingi ili kupata huduma na kupatiwa fursa za Uwezeshaji na hata zinazopatikana katika miradi ya kimkakati.

